- Mwanahabari aliyeangazia stori ya mbunge mchanga zaidi aliyemcharaza mwenyeji wa eneo hilo yu matatani
- Mbunge huyo wa Igembe Kusini anasemekana kumnyeshea Gikunda makonde si haba kwa kuongoza maandamano dhidi yake
Mwanahabari wa shirika la Royal Media Services aliyechapisha taarifa kumhusu mbunge wa Igembe Kusini, aliyenaswa akimnyeshea makonde mwenyeji wa eneo hilo kwa kuandama dhidi yake ametakiwa kufika mbele ya baraza la wazee la Ameru, Njuri Ncheke.
Habari Nyingine: Matukio ya 2017 yamfanya Millie Odhiambo kumwaga machozi Bungeni (Video)
Katika barua iliyoandikwa Mei 5, baraza hilo la Njuri Ncheke tawi la Igembe Kusini iliwataka Mwanahabari wa Royal Media Services Koome Kimenchu, John Gikunda ambaye ni mlalamishi, na Japeth Mutuma aliyedai kushuhudia kisa hicho kufika mbele yake.

Habari Nyingine: Mambo 10 ambayo kila mwanamke anapaswa kuzingatia kabla ya kuolewa
Mbunge wa eneo hilo, John Paul Mwirigi anasemekana kumshambulia Gikunda kwa kuongoza maandamano dhidi yake siku ya Ijumaa, Aprili 27 aliyekuwa akilalamikia hali duni ya barabara katika eneo hilo.
Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka

Habari Nyingine: Otile Brown na Vera Sidika waeka wazi hali yao ya HIV
TUKO.co.ke inafahamu kuwa katibu mkuu wa baraza hilo anapinga kujumuishwa kwa manahabari katika kesi hiyo, akikariri kuwa hiyo ni kinyume na uhuru wa vyombo vya habari.
Read: ENGLISH VERSION
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdibIByf49mrpqylZp6uK2Mo5imoZlixqJ5wKacq61do7e2vshmpZyglaCybsPAprGopZWWeq7DwKeYoZmSlr%2BqecqwmGajpZi1orzIrJ%2BaZaOpvLO1jLKYZqWSqruosYyaoqKlk52us63ZmmSjmZ2Wrm%2B006aj